Waziri wa ulinzi wa Uingereza Ben Wallace ameishutumu Urusi kwa “mipango michafu” na kuomba uchunguzi wa kiulinzi ufanyike kwa kile anachodai kuna mtu alimpigia simu na kujifanya ni Waziri Mkuu wa Ukraine siku ya Alhamis!
Kupitia akaunti yake Twitter aliandika
“Leo jaribio lilifanyika mtu kujifanya waziri mkuu wa Ukraine na kuongea nami. Aliniuliza maswali ya kupotosha na baada ya kumgundua nilikata simu”
Wallace ameishutumu simu hiyo na kuiita mfano wa “Mkakati wa proganda wa urusi, uharibifu na siasa chafu”
Today an attempt was made by an imposter claiming to be Ukrainian PM to speak with me. He posed several misleading questions and after becoming suspicious I terminated the call 1/2
— Rt. Hon Ben Wallace MP (@BWallaceMP) March 17, 2022
Urusi ilituma majeshi yake nchini Ukraine mwezi Februari , ikidai serikali ya Kiev imeshindwa kutimiza makubalaino ya mkataba wa Minsk juu ya ukanda wa Donbass.